Jumla ya Mara Iliyotazamwa

19 Jun 2014

THOMAS MULLER 
Watu hawaangalii umeishi miaka mingapi ila umeleta mabadiliko gani kwenye jamii na ulimwengu mzima.
 Miaka ni namba tu ni kama vile ndani una ndoo kubwa lakini haina maji ila mwenzako mwenye kikombe tu lakini kimejaa maji hivyo mwenye maji ana thamani kubwa sana kuliko asiye na maji, msemo huu utauelewa siku ukiwa na kiu.
 Muller mzaliwa wa 89 mwenye miaka 24 tu lakini ashafanya mambo makubwa kimpira kuliko watu wengi waliostaafu mpira wakiwa na miaka zaidi ya 36.
Dunia nzima macho yetu yapo Brazil licha ya utofauti wa rangi, dini, kabila na itikadi lakini linapokuja suala la kombe la dunia watu wote hujumuika pamoja na ndiyo maana unaambiwa mpira si vita bali burudani.
Si kila timu ishacheza lakini ukianza ushaweka historia, alianza Marcelo kuweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kufunga goli katika mashindano haya ya mwaka 2014 na mchezaji wa kwanza katika historia ya soka kufunga goli la kwanza la kujifunga ingawa ni kwa mabaya lakini mtu ashaandika historia yake na itabaki hivyo vizazi na vizazi.
Robin Van Persie hadi sasa ndiyo kafunga goli bora ambalo hata uwe unamchukia lazima utamani kuwa na mshambuliaji wa aina yake maana kwa lugha ya kigeni wanasema "World Class Player" yaani mchezaji mwenye uwezo wa dunia na mwenye sifa zinazohitajika.
Wapo wengi waliokwisha kuweka rekodi zao ila kwa jana usiku ni THOMAS MULLER ndiye aliyeweka rekodi.
                                           Thomas Mulller - Mshambuliaji wa Ujerumani
Muller ndiye mchezaji wa kwanza kufunga hat trick yaani goli tatu katika mechi moja katika kombe la dunia la mwaka huu kule Brazil hivyo na kumfanya mpaka sasa kuongoza katika orodha ya wafungaji katika mashindano hayo kwa kuwaacha kwa goli moja wanaomfuatia kama vile Robin Van Persie, Neymar pamoja na Karim Benzema.
 Katika fainali za mwaka 2010 kule Afrika ya Kusini, ,uller ndiye alikuwa mfungaji bora wa mashindano yale na kwa jinsi alivyo na uchu wa mabao anaweza kutetea kiatu chake kutokana na kuzungukwa na watu wenye vipaji na viungo bora kabisa ulimwenguni.
Pia Muller bado mabao mawili tu ili awe mfungaji bora wa Ujerumani wa muda wote kitu ambacho ni rahisi sana kwake kukifikisha na sitoshangaa kama atazidi magoli sita zaidi.
Huyu ndiye Thomas Muller Mjerumani mwenye roho ya paka aiyekubali kushindwa ndiyo maana hata klabu yake ya Bayern Munich waligoma kumuuza na kuonmgezea mkataba kutokana na kipaji na umuhimu wake katika klabu.
                                                      SEKI BONIVENTURE KASUGA