Jumla ya Mara Iliyotazamwa

4 Jul 2015

WANAWAKE NA NGUZO YA BEIJING 2015 TUPO TAYARI



kuelekea uchaguzi mkuu tanzania wanawake wengi wamehamasika kugombea nafasi mbalimbali za uongozi bila kujali shughuli wazifanyazo na uzoefu katika vyama mbalimbali vya siasa. rai kwa watanzania na wananchi wote wenye umri wa kupiga kura wachague viongozi wenye uwezo na wanaoweza kuwajibika kwaajili ya wanannchi. sababu sote tunatambua uongozi ni utumwa ,kazi amabayo hazifanani na kazi zingine kwa maana hii basi wagombea wawe wameiva nakuelewa nini utakuwa wajibu wao mara baada yakupata majukumu hayo wasichukulie  uongozi ni kama fursa nyingne na kupata hamasa ya kugombea gombea tu. tujipime na tujisahihishe je tunaweza kuvaa viatu kama vya mama SOPHIA SIMBA ?  ANNNA ABDALAH, tuvuke na ng'ambo kabisa vipi kama nancy pelos, hilaly clinton na wengne wengi . bado mwanamke anayo nafasi ya kuonesha uwezo wake na sio kuatafuta fursa.......................................... ITAENDELA 

manchester city kuwasha moto sokoni pogba na kevin debruyen hudama yao yaitajika


Image result for fabian delphImage result for pogbaImage result for kevin de bruyne            Na Ibrahim kasuga

Man city baada ya kuwashiwa taa ya kijani na UEFA baada ya adhabu yao ya financea fair play kuisha wamewatajaa wachezaji wao wanao wahitaji kwa udi na uvumba kevin de bruyne, raheem sterling na paul pogba hayoo ni majina yanayo husishwa huenda yakaonekana pale Etihad stadium msimu ujao. wakit huohuo kiungo wa timu ya taifa ya uingereza na klabu ya astoni villa Fabian Delph huenda akawa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na man city katika dilisha hili la usajili.

22 Mei 2015

JOSE MOURINHO NA EDEN HAZARD WATWAA TUZO UINGEREZA

Chelsea manager Jose Mourinho celebrates winning the Barclays Manager of the Season Award with his back room team from Stamford Bridge 
Na ibrahim kasuga

Kocha wa Chelsea jose mourinho na kiungo mshambuliaji wa timu hiyo eden hazard wametwaa tuzo ya kocha bora na mcheza bora wa msimu wa 2014-15 katika ligi kuu ya nchini uingereza. Mourinho ameiwezesha Chelsea kuchukua kombe lao la kwanza katika kipindi cha miaka mitano, hazard ameifungia timu yake magoli 14 na pasi za magoli 8.

Jose mourinho amewapiku makocha wa nne katika kinyanganyilo hicho akiwemo arsene wenger wa arsenal, garry monk wa Swansea city, reonald koeman wa saouth amptonton na nigel pearson wa Leicester city
Na hazard ameweza kuchaguliwa kuwa mchezaji bora katika msitu wa wachezaji  nane wakiwemo wachezaji wa 3 kutoka katika klabu yake ya Chelsea ambao ni john terry, cecs fabregas na nemanja matic lakin Sergio aguero wa Manchester city, harry kane wa spurs , alex sanchez wa arsenal na goli kipa wa Manchester united david degea. Kwa upande wa hazard ina kuwa ni tuzo yake ya tutu msimu huu.
Mourinho na hazard wamechaguliwa na kamani maalumu ya wadhamini wa ligi hiyo ambao ni baclays ambao ili wajumuisha waandishi wa habari, wachezaji wa zamani na wadau wa soka.


20 Apr 2015

Tottenham kuwaombea mema Arsenal katika fainali ya FA Cup

Tottenham may want to see Arsene double up.
Ongeza kichwa

 Tottenham sasa wanawaombea Arsenal wawe mabingwa wa FA Cup ile waweze kufuzu kucheza michuano ya ulaya msimu ujao.

Aston Villa wametinga hatua ya fainali ya kumbe la FA Cup ambapo watachuana na Arsenal ambao wanaonekana tayari wananafasi ya kushiriki ligi ya mabingwa barani ulaya(ucl) msimu ujao Aston villa walisha jihakikishia nafasi ya kucheza michuano ya ulaya msimu ujao yani yuropa ligi, lakin kubadilishwa kwa kanuni mwanzoni mwa msimu huu Aston Villa inahitajika wawe mabingwa wa FA Cup iliwaweze kufuzu katika michuano hiyo.
kipindi cha nyuma, kama bingwa wa FA Cup amefuzu kucheza michuano ya mabingwa ulaya(UCL) au yuropa ligi kutokana na nafasi zao katika ligi, mshindi wa pili yani yule aliyepoteza fainali ya FA Cup alikuwa anapewa nafasi ya kucheza yuropa ligi moja kwa moja, baadhi ya vilabu ambavyo vimeshawahi kunufaika na sheria hii ni Southampton(2003), Millwall(2004) na stoke city(2011) hivi karibuni.
Kuanzia msimu wa 2015-16 UEFA yuropa ligi haitaruhusu washindi wa pili wa FA Cup kufuzu katika michuano hiyo, hivyo basi Aton Villa wanahitajika kumfunga Arsenal katika fainali ili waweza kukata tiketi ya kushiriki yuropa ligi msimu wa 2015-16.
kama Arsenal watakuwa mabingwa wa FA Cup nafasi ya mshiriki wa yuropa itakwenda kwa timu itakayo maliza nafasi ya saba(7) katika ligi kuu ya nchini uingereza nasio mshindi wa pili wa FA.
hivyo basi Tottenham ambao wapo nafasi ya sita(6) katika ligi kuu nchini Uingereza ambayo inaelekea ukingoni, kama wakimaliza nafasi ya saba (7) hawana budi kuwaombea mahasimu wao wakubwa Arsenal kuwachapa Astoni villa ili wao waweze kufuzu katika michuano hiyo ya ulaya.





6 Okt 2014

KINANA ATINGA IRINGA, ASEMA UCHAGUZI UJAO WAPINZANI WATAPUKUTIKA


Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akivishwa skafu, baada ya kuwasili kwenye Ofisi ya CCM wilaya ya Iringa Vijijini, leo. Kushoto ni Katibu wa CCM mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga na Wapili kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Isimani William Lukuvi wakati wa mapokezi hayo

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimsalimia Mbunge wa Kilolo Profesa Peter Msola wakati wa mapokezi hayo
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na Kamanda wa UVCCM mkoa wa Iringa, Asas





DIAMOND AFANYA MAKAMUZI YA NGUVU BIG BROTHER HOTSHOTS


Diamond Platnumz akifanya makamuzi ndani ya Big Brother Hotshots. 

STAA wa Bongo Fleva nchini Tanzania, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' usiku huu amefanya makamuzi ya nguvu katika uzinduzi wa shindano la Big Brother Hotshots unaofanyika jijini Johanessburg nchini Afrika Kusini. 

Katika shindano hilo, Tanzania inawakilishwa na watu wawili mrembo Irene 'La Veda' na Idriss. Jumla ya washiriki 26 kutoka mataifa 12 ya Afrika watachuana kwa siku 63 kutafuta mshindi atakayejinyakulia kitita cha dola za Kimarekani 300,000.

UNDANI WA KIFO CHA MKE WA ALICHOKI HUU HAPA ,CHEKI PICHA


Stori: Gladness Mallya
Majonzi! Mkurugenzi wa Bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo’, Ali Choki amepata pigo kubwa la kufiwa na mkewe, Shuea Hamis ‘Mama Shuu’ baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Aliyekuwa mke wa Mkurugenzi wa Bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo’, Ali Choki, marehemu Shuea Hamis ‘Mama Shuu’.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda kwa masikitiko, Choki alisema kwamba mke wake ameugua kwa muda wa miezi tisa akisumbuliwa na tatizo la mguu.
Alisema kwamba katika jitihada za matibabu, mkewe huyo alitibiwa nchini India ikashindikana, akarudishwa nyumbani mpaka mauti yalipomfika usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita.
“Kweli alikuwa akipata mateso makubwa kwani alikuwa hatembei analala tu ndani hivyo kutoa nafasi kwa magonjwa mengine kumshambulia.
“Ukweli nimeumia kwani alikuwa ni mshauri wangu mkuu na ndiye alikuwa kila kitu kwangu.
“Alikuwa akinisapoti sana kwenye kazi yangu ya muziki lakini ndiyo hivyo Mungu amempenda zaidi sina la kufanya,” alisema Choki kwa majonzi.
Ali Choki akiwa kwenye picha ya pamoja na mkewe enzi za uhai wake.
Choki alisema mipango ya mazishi ilifanyika nyumbani kwake tangoma, kigamboni jijini dar na mazishi ya mkewe yalitarajiwa kufanyika jana juma pili sa 10:00 jioni katika Makaburi ya Maduka Mawili, Changombe Dar.