Jumla ya Mara Iliyotazamwa

6 Okt 2014

KINANA ATINGA IRINGA, ASEMA UCHAGUZI UJAO WAPINZANI WATAPUKUTIKA


Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akivishwa skafu, baada ya kuwasili kwenye Ofisi ya CCM wilaya ya Iringa Vijijini, leo. Kushoto ni Katibu wa CCM mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga na Wapili kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Isimani William Lukuvi wakati wa mapokezi hayo

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimsalimia Mbunge wa Kilolo Profesa Peter Msola wakati wa mapokezi hayo
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimiana na Kamanda wa UVCCM mkoa wa Iringa, Asas





DIAMOND AFANYA MAKAMUZI YA NGUVU BIG BROTHER HOTSHOTS


Diamond Platnumz akifanya makamuzi ndani ya Big Brother Hotshots. 

STAA wa Bongo Fleva nchini Tanzania, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' usiku huu amefanya makamuzi ya nguvu katika uzinduzi wa shindano la Big Brother Hotshots unaofanyika jijini Johanessburg nchini Afrika Kusini. 

Katika shindano hilo, Tanzania inawakilishwa na watu wawili mrembo Irene 'La Veda' na Idriss. Jumla ya washiriki 26 kutoka mataifa 12 ya Afrika watachuana kwa siku 63 kutafuta mshindi atakayejinyakulia kitita cha dola za Kimarekani 300,000.

UNDANI WA KIFO CHA MKE WA ALICHOKI HUU HAPA ,CHEKI PICHA


Stori: Gladness Mallya
Majonzi! Mkurugenzi wa Bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo’, Ali Choki amepata pigo kubwa la kufiwa na mkewe, Shuea Hamis ‘Mama Shuu’ baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Aliyekuwa mke wa Mkurugenzi wa Bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo’, Ali Choki, marehemu Shuea Hamis ‘Mama Shuu’.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda kwa masikitiko, Choki alisema kwamba mke wake ameugua kwa muda wa miezi tisa akisumbuliwa na tatizo la mguu.
Alisema kwamba katika jitihada za matibabu, mkewe huyo alitibiwa nchini India ikashindikana, akarudishwa nyumbani mpaka mauti yalipomfika usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita.
“Kweli alikuwa akipata mateso makubwa kwani alikuwa hatembei analala tu ndani hivyo kutoa nafasi kwa magonjwa mengine kumshambulia.
“Ukweli nimeumia kwani alikuwa ni mshauri wangu mkuu na ndiye alikuwa kila kitu kwangu.
“Alikuwa akinisapoti sana kwenye kazi yangu ya muziki lakini ndiyo hivyo Mungu amempenda zaidi sina la kufanya,” alisema Choki kwa majonzi.
Ali Choki akiwa kwenye picha ya pamoja na mkewe enzi za uhai wake.
Choki alisema mipango ya mazishi ilifanyika nyumbani kwake tangoma, kigamboni jijini dar na mazishi ya mkewe yalitarajiwa kufanyika jana juma pili sa 10:00 jioni katika Makaburi ya Maduka Mawili, Changombe Dar.

27 Sep 2014

PRESIDENT KIKWETE VISITS CNN STUDIOS IN NEW YORK


President Jakaya Mrisho Kikwete chats with  Cable News Network (CNN) 's Richard Quest and Maggie Lake when he visited  CNN Studios at the  Time Warner Cente in New York.  
CNN is an American basic cable and satellite television channel that is owned by the Turner Broadcasting System division of Time Warner. 
The 24-hour cable news channel was founded in 1980 by American media proprietor Ted Turner.  Upon its launch, CNN was the first television channel to provide 24-hour news coverage, and was the first all-news television channel in the United States.
While the news channel has numerous affiliates, CNN primarily broadcasts from its headquarters at the CNN Center in Atlanta, theTime Warner Center in New York City, and studios in Washington, D.C. and Los Angeles. CNN is sometimes referred to as CNN/U.S. to distinguish the American channel from its international sister network, CNN International.
President Jakaya Mrisho Kikwete poses with CNN's Richard Quest and Maggie Lake when he visited CNN Studios at the Time Warner Building in New York
President Jakaya Mrisho Kikwete presents  CNN's Richard Quest when he visited CNN Studios at the Time Warner Building in New York. Right Ms. JulietRugeiyamu Kairuki, the Executive Director of the Tanzania Investment Centre. The Tour was jointly organized by the TIC and CNN as part of an on going partnership to promote Tanzania  as an attractive destination for investment and tourism. 
They also discussed  the forthcoming African Journalist of the year Awards Ceremony to be held in Dar es salaam later this year.
President Kikwete and his entourage take a souvenir photo in the CNN Studios during his visit
President Jakaya Mrisho Kikwete and  CNN's Richard Quest and Maggie Lake when he visited CNN Studios at the Time Warner Building in New York.  This is where Richard Quest produces his world famous "Quest Means Business Programmes"
President Jakaya Mrisho Kikwete and his entourage are given a guided tour by  CNN's Richard Quest when he visited CNN Studios at the Time Warner Building in New York.  
President Jakaya Mrisho Kikwete and his entourage are given a guided tour by  CNN's Richard Quest when he visited CNN Studios at the Time Warner Building in New York.  
President Jakaya Mrisho Kikwete and his entourage in talks with Mr.  Ken Jautz (second left), the  Executive Vice President of CNN (Responsible for CNN/US) and Mr. Rani Raad (left  Executive Vice President & Chief Commercial Officer (CNN International) when he visited CNN Studios at the Time Warner Building in New York.  The  CNN .executives engaged President Kikwete  on Tanzania's a investment Track record and the country's  impressive economic performance, as well as its  approach to responsible Journalism
 CNN memorabilia and TIC's promotional banner  on display during President Kikwete'svisit of  CNN studios in New York. STATE HOUSE PHOTOS

KINANA AMALIZA ZIARA YAKE KOROGWE




 Katibu  Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishona nguo kwenye ofisi ya Veronica Simba (kushoto) iliyopo Mombo Sokoni,kulia ni Mbunge wa Korogwe Vijijini Ndugu Stephen Ngonyani ,Katibu Mkuu alikuwa kwenye ziara ya siku moja katika wilaya ya Korogwe Vijijini ambapo licha ya kukagua miradi mbali mbali ya ujenzi wa maabara na ofisi za CCM alipata nafasi ya kuwahutubia wananchi na kuwasikiliza  .

  Katibu  Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimuelekeza Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kushona nguo kwenye ofisi ya Veronica Simba (kushoto) iliyopo Mombo Sokoni.
 
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Ueneziwakinunua matunda kabla ya kwenda kwenye mkutano wa hadhara Mombo.


 Diwani wa kata ya Mombo akishangiia baada ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kutamka wazi kuwa katika kuhakikisha wanapata halmashauri ya mji mdogo.
 Mama akiwa amembeba mwana ili awaone viongozi wake vizuri kwenye uwanja wa mikutano Mombo ambapo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alihutubia.
 Wananchi wakiwa wamekaa kwa shauku ya kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCm Ndugu Abdulrahan Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kulia) akiwapungia watu wakati wa kuwasili kwenye uwanja wa mikutano mjini Mombo akiwa pamoja  na Katibu wa NEC Itikadi Nape Nnauye
 Katibu Mkuu akiwapugia watu waliojazana kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mombo
 Umati wa wakazi wa Mombo uliojitokeza kwenye Mkutano wa Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Mombo ambapo aliwaambia wananchi hao wanachofanya wapinzani ni biashara, kwani kwao kuandamanisha watu ni mtaji mzuri wa kuwaingizia pesa kutoka nje.

 Umati wa watu ukimsikiliza Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na na Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Tanga Aisha Kigoda pamoja na Mjumbe wa NEC wilaya ya Korogwe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi mkoani Tanga Dk. Edmund Mdolwa wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Mombo.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Mombo.
Wananchi wakifuatilia mkutano wa Kinana mjini Mbombo
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amekaa kwenye kiti tayari kupokea zawadi kutoka kwa wamasai wanaoishi Mombo.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokea zawadi kutoka kwa wamasai wa Mombo.
 Katibu wa CCM Ndugu Abdulrahman akipeana mkono wa shukrani kwa kiongozi wa wamasai wa Mbombo Samng'o Maikaambaye [ia ni mwenyekiti wa Tawi la Chang'ombe ,Mombo. na Sufyan Omar

26 Sep 2014

KINANA AACHA GUMZO KOROGWE MJINI


  • Ashiriki kuchavanga kwenye shamba la Skimu ya Mahenge
  • Nape awafungua vijana kuhusu siasa zisizo na tija 
  • Mrisho Gambo awa shujaa kwa kusema ukweli kwenye kila hoja iliyoletwa na wananchi wa Korogwe.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kulima shamba la mpunga kwenye mradi wa kilimo kwanza wa Skimu ya Mahenge.
 Mifereji ya maji kwenye shamba la skimu ya Mahenge

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akishiriki kufyeka majani kwenye eneo la soko la sabasaba mjini Korogwe.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akishiriki kujenga zahanati Mahenge kwa Mndolwa.
Mbunge wa Korogwe mjini Bw. Yusuph Nassir akielezea mipango ya maendeleo ya jimbo lake wakati wa kukagua maendeleo ya ujenzi wa zahanati ya Mahenge Kwamndolwa .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa vyumba vya maabara vya shule ya sekondari ya Old Korogwe.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa Korogwe kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mazoezi ambapo aliwaasa vijana kuwa makini na wanasiasa wanaotanguliza madaraka kuliko utu.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimia wakazi wa Korogwe walifurika kwenye mkutano wa hadhara ambapo aliwaambia wananchi hao kuchagua viongozi bora kwenye chaguzi zote zijazo,kuhakikisha watoto wao wanaenda shule na wasirudishwe kwa sababu ya ada na mwisho aliwasisitiza wakazi wa Korogwe kujiunga na mifuko ya Afya ya jamii.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mheshimiwa Mrisho Gambo kusalimia wananchi wa Korogwe wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Msingi ya Mazoezi.
 Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mheshimiwa Mrisho Gambo akiwahutubia wakazi wa Korogwe wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya Msingi ya Mazoezi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Korogwe kwenye mkutano uliokuwa na umati mkubwa wa watu waliokuwa na shauku ya kuuliza maswali kuhusu maendeleo yao ya Korogwe.
(Picha na Adam Mzee) na Sufyan Omar