Jumla ya Mara Iliyotazamwa

13 Sep 2014

KINANA AANZA ZIARA MKOA WA PWANI, AHUTUBIA MAMIA YA WATU KIMANZICHANA LEO


Katibu Mkuu wa CCM, akihutubia mamia ya wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika leo, Kimanzichana, wilayani Mkuranga, mwanzoni mwa ziara yake mkoa wa Pwani.

TMF YATOA SHS. 1.7 BILIONI KWA VYOMBO VYA HABARI


Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF), Ernest Sungura

NA BEATRICE SHAYO


Katika kuendeleza habari za uchunguzi nchini Mfuko wa vyombo vya habari (TMF) umetoa ruzuku ya Sh. bilion 1.7 kwa vyombo vya habari 16.
Mkurugenzi wa TMF, Ernest Sungura, alisema jana wakati wa kutia saini mkataba wa mwisho wa kutekeleza makubaliano ya kufanya habari za uchunguzi nchini.
Sungura alisema ruzuku hiyo inatakiwa kutumiwa kwa malengo yaliyokusudiwa na kwamba wamewaweka wakaguzi wao wa ndani watakaokagua mara kwa mara. 
“Ruzuku hiyo imetokana na msaada wa kodi za wananchi kutoka nchi za Denmark, Swissland, Norway na Uingereza kwa ajili ya kutatua matatizo yaliyopo hivyo inatakiwa kuzithamini na kuweka nidhamu kubwa,” alisema.
Sungura alisema, kwa atakaye fuja au kutumia vibaya ruzuku hiyo atakuwa anajitafutia ubaya na kwamba hatapata tena nafasi ya kupata ruzuku hiyo ambayo hutolewa kila mwaka.
Aidha, alisema jamii ipo katika changamoto kadhaa hali ambayo inasababisha maisha ya watu kutobadilika, vyombo vya habari vinatakiwa kuliangalia suala hilo katika kuibua mambo mbalimbali ili kuwepo na mabadiliko.
Alisema mahitaji muhimu ya binadamu hayapatikani katika jamii ikiwamo huduma za afya, shule na vitu vingine vya muhimu vimekuwa havipatikani kutokana na changamoto za tabia za kibadhirifu.
Aliongeza kuwa vyombo vya habari vinahesabiwa kuwa ni muhimili ambao siyo rasmi wakati ni muhimili muhimu unaofanya kazi kubwa na kuibua mambo mbalimbali yakiwamo ya ufisadi.
Aidha, alisema mkakati wao ni kuendelea kuviwezesha vyombo vya habari katika kuibua maovu ndani ya jamii, ili changamoto hizo ziweze kufanyiwa kazi.
Ruzuku hiyo imegawanywa katika makundi mbalimbali na kwamba chombo cha habari kilichopata ruzuku kubwa ni Sh. milioni 185 na cha mwisho kimepata Sh. milioni 50.
CHANZO: NIPASHE

10 Sep 2014

WATOTO 808,111 KUFANYA MTIHANI WA DARASA LA SABA LEO

Jenista Mhagama, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi

Jumla ya watahiniwa 808,111 wanatarajia kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi leo, huku kati ya hao wavulana ni 378,470 sawa na asilimia 46.84 na wasichana ni 429,641  (asilimia 53.16).

Aidha, katika mtihani huo, watahiniwa 783,223 watafanya mtihani kwa lugha ya Kiswahili, watahiniwa 24,888 watafanya mtihami kwa lugha ya Kiingereza.

Kwa upande wa wasioona walioandikishwa kufanya mtihani ni 86 , wavulana 54 na wasichana 32, na watahiniwa wenye uoni hafifu wanaotarajiwa kufanya mtihani huo ni 714, kati yao  wavulana ni 371 na wasichana 343.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Jenista Mhagama, alisema maandalizi yote kwa ajili ya mtihani yameshakamilika ikiwa ni pamoja na kusambazwa kwa karatasi za mitihani, fomu maalum za OMR za kujibia mitihani pamoja na nyaraka zote muhimu zinazohusu mtihani huo.

Mhagama alisema mtihani mtihani huo ni muhimu kwa taifa, wazazi na jamii kwa ujumla na kwamba masomo yatakayotahiniwa ni Kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na Maarifa ya Jamii  mtihani ambao utafanyika kwa siku mbili mfululizo.

Alitoa wito kwa kamati za mitihani za mikoa na wilaya kuhakikisha taratibu zote za mitihani zinazingatiwa ipasavyo na kuwataka wasimamizi, walimu, wananchi na wanafunzi  kutoshiriki katika vitendo vya udanganyifu na kwamba atakayebainika atachukuliwa hatua kali za kisheria.
CHANZO: NIPASHE   

NDOA YA LUCY KOMBA MIKOSI 3


ILE ndoa iliyokuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu ya nyota wa filamu Bongo, Lucy Francis Komba na mzungu wake raia wa Denmark anayejulikana kwa jina moja la Janus hatimaye imefungwa na kutawaliwa na matukio yenye mikosi kibao.
Nyota wa filamu Bongo, Lucy Francis Komba na mzungu wake raia wa Denmark anayejulikana kwa jina moja la Janus wakiwa ni wenye furaha wakati wa harusi yao.
Ndoa hiyo ilifungwa Jumamosi iliyopita kwenye Kanisa la Roman Katoliki Parokia ya Mtakatifu Benedict lililopo maeneo ya Kurasini- Bandari jijini Dar.
Baada ya zoezi hilo kumalizika, wawili hao na wapambe wao walikwenda katika Kisiwa cha Bongoyo, Dar kwa ajili kupiga picha za ukumbusho. Kisiwa hicho kipo Kilomita 2.5 kutoka Pwani ya Jiji la Dar.
Mdenmark Janus akimwelekeza jambo mke wake rasmi Lucy Francis Komba.
Hata hivyo, zoezi la kwenda kupiga picha kwenye kisiwa hicho liliingia mkosi kufuatia maharusi hao kupanda  boti maeneo ya Slip Way, Oysterbay, Dar na kupigwa na mawimbi makubwa yaliyowafanya watumbukie baharini kabla ya kuokolewa na wapiga mbizi mahiri.
“Jamani sijui balaa gani hili? Yaani tumetumbukia baharini tukienda Bongoyo, viatu vimezama, nguo tulizovaa zimelowa,  tukaletewa nyingine, simu yangu pia iliingia majini lakini tunamshukuru Mungu tuliokolewa na kuendelea na safari,”alisema Lucy alipoulizwa na gazeti hili.
Wapambe wakijipanga kutoa sapoti katika harusi hiyo.
Lucy alisema walifika salama kisiwani Bongoyo na kupiga picha mbalimbali za ukumbusho na baada ya kumaliza walianza safari ya kurejea mjini ili kwenda kula na watoto yatima wa Kituo cha New Life kilichopo Kigogo jijini Dar lakini wakapata mkosi wa pili.
Lucy alisema hajui ni nini, kwani alishangaa sana baada ya kutoka Bongoyo wakiwa maeneo ya Kinondoni kuna gari lililoonekana kuwafuatilia toka mbali, liliwafikia na kuligonga gari lililokuwa katika msafara wake waliokuwa wakichukua matukio kwa kamera ya video, wakashuka na kuanza kuwafanyia fujo kisha wakawapora kamera hiyo na kuondoka kwa kasi eneo hilo.
Wanaharusi Lucy Komba na mumewe Janus wakipozi kupata picha ya ukumbusho.
“Sijajua mpaka sasa wale watu ni akina nani na walikuwa na dhamira gani, sijui walitumwa? Nashindwa kuelewa maana walikuwa mabaunsa wawili na mwanamke mmoja,” alisema Lucy.
Mbali na misukosuko yote waliyopata siku hiyo, lakini maharusi hao walifanikiwa kufika katika Ukumbi wa Makumbusho uliopo Posta Mpya, Dar ambapo sherehe ya kifahari ilifanyika na kuhudhuriwa na marafiki wa bi harusi na viongozi kutoka serikalini.
Mbali na yote, shughuli hiyo ilikuwa na vituko mbalimbali ambavyo viliwakosha waalikwa, ikiwemo watu wa kareti kutoa salamu zao za kikomandoo, mtu wa mazingaombwe ya nyoka, wanenguaji kutoka Kampuni ya Bia ya Windhoek kutoa shoo ya nguvu na msanii mkongwe Bongo, Ummy Wenceslaus ‘Dokii’ kutumbuiza.
Maharusi wakiingia katika Ukumbi wa Makumbusho ulio Posta kwa ajili ya sherehe.
Bwana harusi naye alionesha mila ya kikwao kwa kulazwa chini na kuvuliwa viatu kisha kuvalishwa tena ikiwa ni ishara kwamba ameagana na ukapera.
Msanii huyo alipata zawadi kedekede kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki zake. Mama yake mzazi aliyekuwa Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi, Ilala, Marietta Minangi  alimzawadia kiwanja kilichopo Bunju jijini Dar huku baba yake mdogo (jina halikupatikana) akimpa mbuzi na ng’ombe wawili wa maziwa.Kaka yake alimkabidhi shilingi milioni tisa taslimu ukumbini hapo na kamati ya sherehe ilimpa shilingi milioni tatu bila kumsahau Dokii ambaye alimzawadia matofali 500 na mifuko 10 ya simenti.
Kutokana na thamani kubwa aliyonayo mzazi wake kwa kumzaa na kumlea vyema, Lucy alimfanyia ‘sapraizi’ mama yake huyo kwa kumpa zawadi ya gari aina ya Toyota Prado ambalo alimkabidhi mahali hapo.
“Namshukuru sana mama yangu kwa malezi mazuri aliyonipa mpaka sasa nimeolewa, sioni cha kumlipa kwa thamani kubwa aliyonayo kwangu, ila nimeamua kumzawadia gari aina ya Prado, japo ana gari lakini nimemzawadia hili ikiwa kama upendo wangu kwake,”alisema Lucy ambaye siku si nyingi anataraji kuondoka nchini kwenda Denmark kwa mumewe.

KAJALA APAGAWA NA FEDHA, AVUNJA REKODI YA WEMA SEPETU,ATOA KUFURU YA MWAKA SOMA MKASA MZIMA HAPA


FEDHA mwanaharamu! Katika hali ya kushangaza, staa wa filamu ambaye fedha imemtembelea kwa sasa, Kajala Masanja ‘K’ amenaswa akimwaga fedha kama amechanganyikiwa mbele ya kadamnasi, Risasi Mchanganyiko linakupa mchapo kamili.
Staa wa filamu, Kajala Masanja ‘K’ akiwatunza wakali kutoka Yamoto Band.
Tukio hilo lililowaacha watu midomo wazi lilitokea hivi karibuni katika Viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar, kulipokuwa na uzinduzi wa filamu ya Mateso Yangu Ughaibuni ambapo muigizaji huyo alionesha jeuri ya fedha baada ya kupagawishwa na sebene la Yamoto Band.
ALIINGIA NA WAPAMBE
Awali, paparazi wetu alimshuhudia Kajala akitinga viwanjani hapo akiwa ameongozana na wapambe takriban 15 na kwenda kukaa katika meza moja ambapo mhudumu aliwasikiliza kujua wanachokunywa.
VINYWAJI VYAAGIZWA NJE
Kutokana na uzinduzi huo kutokuwa na pombe, K aliamuru kila mtu aletewe kile anachokihitaji halafu bili yote apelekewe yeye, Mama la Mama kama wanavyowaita watoto wa mjini.
“Waletee hawa vinywaji wanavyojisikia kunywa pia wasikilize meza ile pale kisha bili niletee mimi,” alisikika Kajala.
Mama wa Wamama 'Kajala' akirudi kukaa mara baada ya kuwatunza wakali wa Yamoto Band.
MINONG’ONO YAMTIA WAZIMU
Baada ya kauli ile wafuatiliaji wa mambo ya watu hasa wakienda shughulini wakaanza kutoa minong’ono kuwa hata iweje bado Kajala hajafikia uchezeaji wa fedha kama alivyokuwa shosti wake wa ‘long time’, Wema Sepetu aliyepewa taito ya Madam kutokana na kujua kuzitumbua fedha.
“Kwani kuagizia watu vinywaji ndiyo kuonyesha kufuru au jeuri ya fedha, angalia wahudumu wanavyogawa vinywaji kwa kusuasua, unafikiri angekuwa Madam (Wema) angekubali hata akae muda wote asiende kutunza thubutu, chezea Madame (Madam) wewe,” alisikika mualikwa mmoja.

Kajala akiserebuka na Mwanyekiti wa Bongo Muvi, Steven Mengere 'Steve Nyerere'.
YAMOTO BAND WAMWINUA
Ndani ya muda mfupi, Kajala akavunja ukimya baada ya bendi ya Yamoto kupiga wimbo wa Nitajuta ndipo Kajala aliposhindwa kuvumilia na kwenda kuwamwagia fedha huku wapambe wake wakimshangilia.
“Ndiooo mkurugenzi hivyo ndivyo ujana unavyoliwa,” kelele zilisikika kutoka katika meza waliyokuwa wameketi wapambe wake.
KAMA LAKI SITA NA USHEE
Ufukunyuzi wa paparazi wetu kwa harakaharaka, ulizihesabu fedha hizo alizowamwagia watoto hao wa Mkubwa Fella ambapo hesabu zilionesha zilikuwa zaidi ya shilingi laki sita.
Mama wa Wamama 'Kajala' akiwa na shosti yake 'Odama'
AKOSOLEWA
Hata hivyo kuna baadhi ya watu walimkosoa staa huyo kwa kusema kitendo cha yeye kupata fedha kwa sasa kinaonekana kumchanganya kiasi cha kuzimwaga pasipo kuwa na sababu ya msingi.
“Bora angetunza kidogo na nyingine akatumia kwa vitu vya maana likiwemo suala la kumsaidia mume wake ambaye yuko jela kwa kushindwa kulipa faini ya shilingi mil. 200,” alisikika mdau mmoja wa filamu ambaye hakutaka kuanikwa jina gazetini.
UZALENDO WAMSHINDA STEVE NYERERE
Kadri Kajala alivyozidi kumwaga fedha, uzalendo ulimshinda Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ ambapo alimfuata Kajala na kutaka na yeye amtunze.
“Hebu kuwa na adabu, mi mkubwa wako na mimi nitunze kwanza mambo mengine yaendelee, haiwezekani uoneshe jeuri ya fedha kiasi hiki wakati mimi mdau nipo hapa hunipozi,” alisikika Steve Nyerere.
AMEZIPATA WAPI FEDHA?
Baada ya vurugu zote zile kufanyika, paparazi wetu alimvaa Kajala na kutaka kujua vyanzo vya fedha hizo na kumuuliza kama amehongwa, akachomoa.
“Mimi sihongwi ukitegemea fedha za mwanaume huwezi kuwa na heshima mjini, nina biashara zangu na kampuni yangu hiki ninachokitumia hapa ni faida tu ya siku mbili tatu mimi mjasiriamali wewe,” alisema Kajala.
TUJIKUMBUSHE
Kumbukumbu zinaonesha, kipindi ambacho Kajala na Wema walikuwa marafiki, Kajala hakuwa na fedha nyingi lakini baada ya kutofautiana, pesa imemtembelea huku mwenzake akidaiwa kuyumba kiuchumi.

Mjadala: kifanyike nini kupunguza ama kukomesha ajali barabarani??


Taswira hii inayosambaa kila pembe katika mitandao ya jamii na Globu ya Jamii kuipata ndiyo chachu ya mjadala wetu ambao mdau unaombwa kuchangia bila kuchafua hali ya hewa. Ukweli ni kwamba THIS IS TOO MUCH! Ni lazima kifanyike kitu ama lifanyike jambo kukomesha maafa ya kila mara nchini kutokana na ajali za barabarani.

10 Things you Didn't know about Germany's star coach Joachim Loew


 As celebrations in Germany begin and fans express their love (or loew) for the man, here are 10 things to know about Joachim Loew.
1. Understanding the vitals

Joachim Loew was born in Schonau, West Germany on Feb 3, 1960. Standing tall at 182 cm - he is German, after all - the 54-year-old looks good for a middle-aged man.

Also, Joachim Loew is pronounced yoa-kim-luv, so now we can declare his name loud and proud.

2. A serious coach with a cute nickname

Loew is nicknamed Jogi, a shortened version of his first name Joachim. It certainly has no reference to a certain comic book and cartoon-animated bear, but we think that's rather cute for a serious football coach.

3. Sorry single ladies, someone has already put a ring on it

Loew is married to 52-year-old Daniela Loew, and the pair have been together for over 27 years. They have no children. Props to the guy for sustaining his marriage as well as his football team.

Their love story is also a sweet one. The couple reportedly met in 1978 when he was 17 and she was 15, when he was a soccer player with German club SC Freiburg. They had dated for eight years before tying the knot.

4. He has a massive annual salary

Loew's annual salary is a staggering US$3.6 million (S$4.5 million), 82 times more than the average person in Germany. He also has a net worth of US$18 million (S$22.4 million).

This makes him one of the highest-paid national football team coaches in 2014. Judging by his coaching success, we think he very well earned it.

5. An ex-football player with a broken dream

Loew was a football player with SC Freiburg from 1978 to 1980 and from 1985 to 1989. He was displaying exceptional talent as a young amateur player, and by the age of 18 had obtained his first professional contract.

Unfortunately, a broken shin bone at the age of 22 dashed his hopes of making it to the top. Loew then decided to become a coach, studying the game on and off the field.

6. He rose to fame as a national football coach

Loew joined the German national football team as assistant coach in 2004, alongside Jurgen Klinsmann. The pair led the team in the 2006 World Cup to win all three games in their group and finish third after beating Portugal.

When Klinsmann decided not to extend his contract with the team, Loew took over the position of head coach. With one of the youngest squads on the field, he led the German national team to a third place finish in the 2010 World Cup and finally, to championship victory in 2014.

7. Dressed by Hugo Boss like a true German boss

So he has made it onto the good-looking and the richest list, but the high-achieving Loew is not leaving himself out of the best-dressed group.

His trademark outfit was a lucky blue cashmere sweater at the 2010 World Cup. This year, thanks to Hugo Boss, he adopted a minimalist style with a simple collared shirt and slim-cut pants.

Casual and cool with just a tinge of sleek sophistication, Loew looked clean and sharp at every game, just like his German team.

8. Loved on the field, banned from the wheel

Banned from driving for six months for clocking up too many points on his licence, the German coach did not drive in Brazil for the World Cup at all.

According to German newspaper Die Welt, he has been frequently caught speeding and using his mobile phone at the wheel.

Germany's general manager Oliver Bierhoff had joked that he will "talk with our sponsors Mercedes-Benz to see if they can provide him a car with a speed limiter".

9. Not a straight-laced coach, but not gay either

Loew had dismissed rumours of him being gay in 2011, when the German daily paper Die Welt asked him if he was "grouped with the gay half" of the national football team.

This was in reference to Oliver Bierhoff's, Germany's team manager, previous comments that "half the national team is supposedly gay, including the training staff".

In reply to the paper, Loew said, "Feel free to ask my wife".

10. The hair is real

There were rumours in Germany several years that his thick mop of black hair is actually a wig, but in an interview with Die Welt, Loew regarded the rumour as "rubbish". He even offered the reporter to tug on his hair.

There is even a facebook group dedicated to the black luscious locks of the German coach, titled "How awesome is Joachim Loew's hair?"

Loew has never disclosed how he manages to maintain his perfect crop of hair. We can only speculate that he dries or dyes it regularly.

RAIS YOWERI MUSEVENI AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA SIKU MOJA

 Rais wa Uganda Yoweri Museveni akiteremka katika ndege iliyomleta leo jijini dar es Salaam kwa ajili ya  ziara yake ya siku moja nchini Tanzania .

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akikagua Gwaride la Maaskari pamoja na Mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni baada ya kuwasili  leo jijini  katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa Mwalimu Julius Nyerere kwa ajili ya ziara ya siku moja.

8 Sep 2014

Historia ya Noti ya Tanzania

Kwa muda mrefu fedha zilizotumia katika nchi hii zilikuwa ni sarafu. Noti za karatasi zilianza kutumika mwaka 1905 wakati wa Utawala wa Mjerumani kwa upande wa Tanganyika (Tanzania Bara). Noti hizo zilitolewa katika thamani ya Rupie 5, 10, 50, 100 na Rupie 500 kama ionekanavyo hapa chini. Noti za Rupie 500 zilikuwa chache sana na sikufanikiwa kupata picha yake.

Rupie 5


Rupie 10


Rupie 50


Rupie 100


Kwa upande wa Zanzibar, mwaka huo huo wa 1905, noti za Rupee za Kizanzibari zilitolewa katika thamani za Rupee 5, 10, 20, 50, 100 na Rupee 500 pia. Kwa bahati mbaya sikuweza kupata picha zake zote, naonyesha mfano wa noti za Rupee 5 tano tu niliyofanikiwa kupata.

5 Zanzibar Rupee



Wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, Serikali ya Kijerumani ilitoa noti za dharura ambazo zilikuwa ni za karatasi ya kawaida kabisa. Noti hizi zilikuwa katika thamani za Rupie 1, 5, 10, 20, 50 na Rupie 200 ingawa hizi za Rupie 200 zilikuwa adimu sana na sikufanikiwa kupata picha yake.

1 Rupie


5 Rupien


10 Rupien


20 Rupien


50 Rupien


Noti hizi za dharura zilikuwa hafifu sana na wakati mwingine zilikuwa zinafyatuliwa kwa muhuri tu kama hii hapa chini ya Rupie 1.


Inaelekea kuwa Mji wa Tabora ulikuwa na umuhimu wa pili kwa Dar es Salaam wakati wa Serikali ya Kijerumani kwa vile unaonyeshwa katika Noti zote. Kama mtakumbuka, ile sarafu ya dhahabu ya Rupie 15 ilikuwa inaitwa "Tabora Pound."


Wakati wa Utawala wa Mwingereza

Baada ya Utawala wa Kijerumani kuanguka na nchi kuchukuliwa na Waingereza mwaka 1920, kwanza nchi ilitumia Noti za Rupee za Afrika ya Mashariki na Rupee za Zanzibar ingawa Rupie za Kijerumani pia ziliendelea kutumika. Kwa upande wa Zanzibar Noti ya Rupee 1 ilianzishwa mwaka 1920. Baadhi ya noti hizo ni hizi hapa:

1 Zanzibar Rupee



1 EA Rupee



5 EA Rupee



10 EA Rupee



Katikati ya mwaka 1920, Serikali ya Uingereza ilianzisha sarafu ya pamoja kwa nchi zote za Afrika ya Mashariki iliyojulikana kama Florin ya Afrika ya Mashariki. Noti za Florini zilikuwa katika thamani za Florin 1, 5, 10, 20, 50, 100 na Florin 500, ambapo noti za kuanzia Florin 10 na kuendelea juu zilikuwa pia na thamani ya Pound (1, 2, 5, 10 na 50). Kwa vile sarafu hii haikudumu zaidi ya miezi sita, ni noti chache sana zilizotolewa, mifano ya noti hizo ni kama ifuatavyo:

1 EA Florin


5 EA Florin


Mwanzoni mwa mwak 1921, Serikali ya Kiingereza ilianzisha sarafu ya pamoja Afrika Mashariki iliyojulikana kama Shilingi ya Afrika ya Mashariki na hivyo kuondokana na Florin ya Afrika Mashariki. Shilingi ya Afrika Mashariki (baadaye nitakuwa naandika kwa kifupi tu kama Shilling) ilikuwa na thamani ya Shilingi 20 kwa Pound moja na ilikuwa imeegeshwa kwenye Pound kiasi kuwa thamani ya Shiling 20 kwa Pound haikubadilika (Hii ndiyo sababu Watanzania tuliendelea kuiita shilingi 20 kama 'Pound'). Noti za Shilingi zilizotolewa wakati huo zilikuwa za thamani za Shilingi 5, 10, 20, 100, 1,000, na Shilingi 10,000. Noti za Shilingi ishirini na kuendelea juu zilikuwa pia na thamani ya Pound (1, 5, 50). Noti hizi zilikuwa zimeandikwa kwa Kiingereza, Kiarabu na Kiamhara kinachotumika Ethiopia. Katika utawala wote wa Kiingereza, kulitolewa mitindo miwili tu ya noti hizo. Mtindo wa kwanza ulidumu kuanzia mwaka 1921 hadi mwaka 1958, ma mtindo wa pili ulidumu kuanzia mwaka 1958 hadi baada ya Uhuru mwaka 1964. Sura ya mbele ya noti zote ilikuwa ikionyesha Mtawala wa Himaya ya Uingereza. Sura ya nyuma kwa upande wa noti za mtindo wa kwanza ilikuwa na simba mmoja wa kiume katika eneo la Mlima Kenya. Noti zilizotolewa mara ya kwanza wakati wa Utawala wa Mfalme George wa Tano (1910-1936) ni kama ifuatavyo:

5 EA Shilling


10 EA Shilling


20 EA Shilling


100 EA Shilling


1,000 EA Shilling

(Picha hii ilipingwa wakati pesa imeshafutwa rasmi kwa kutobolewa matundu; noti halisi haikuwa na matundu hayo)
Kwa thamani ya shilingi na uchumi wa watu wakati huo, ni noti chache sana zenye thamani ya Shiling 1,000 na Shilingi 10,000 ziliingia kwenye mzunguko, na sikufanikiwa kupata noti ya Shilingi 10,000. Kwa hiyo ilipofika mwaka 1933, serikali ikaamua kusimaisha matumizi ya noti za Shilingi 1,000 ingawa zile za Shilingi 10,000 ziliendelea. Wakati wa utawala mfupi wa Mfalme Edward wa Nane mwaka 1936, hazikutolewa noti zozote. Noti nyingine zilitolewa wakati wa utawala wa Mfame George wa Sita (1936-1952), ambapo noti ya Shilingi 1 ilianzishwa. Noti hizo zilikuwa kama ifuatavyo.

1 EA Shilling


5 EA Shilling


10 EA Shilling


20 EA Shilling


100 EA Shilling


Kutokana na uadimu wake, sikuweza kupata noti za Shilingi 10,000. Hata hivyo miaka 11 ndani ya utawala wa Mfalme George wa Sita, iliamuliwa kufuta noti hizi za Shilingi 10,000 ambazo zilikuwa hazitumiki sana.

Baada ya kifo cha Mfalme George wa Sita mwaka 1952 na binti yake Malkia Elizabeth wa Pili kuchukua usukani noti zilizotolewa zilikuwa zinafanana na zile zilizokuwapo mwanzoni isipokuwa aliondoa noti ya Shilingi 1 kwenye mzunguko.

5 EA Shilling


10 EA Shilling


20 EA Shilling


100 EA Shilling




Mwishoni mwa Utawala wa Kiingereza

Hata hivyo, mwaka 1958, noti hizo zilitengezwa upya katika mtindo tofauti na zile zilizokuwapo mwanzo. Noti mpya zilikuwa na rangi nyingi huku zikionyesha mazao mbali mbali ya uchumi yaliyokuwepo Afrika ya Mashariki. Noti ya Shilingi 5 ilionyesha pamba na karafuu; noti ya Shilingi 10 ilionyesha mkonge na chai; noti ya Shilingi 20 ilionyesha kahawa na alizeti, na mwisho noti ya Shilingi 100 ilionyesha minazi, miwese na pareto. Inaelekea kuwa kuanzia hapo, shilingi ya Afrika Mashariki iliacha kubebeshwa kwenye pound kwa vile noti mpya hazikuwa na thamani ya pound tena.

5 EA Shilling


10 EA Shilling


20 EA Shilling


100 EA Shilling


Noti hizi ziliendelea hadi baada ya Uhuru ingawa mwaka 1961 zilifanyiwa marekebsihao madogo kwenye sura ya mbele ili kuweza kuonyesha sahihi sita za Wajumbe wa Bodi ya Fedha ya Afrika Mashariki ambapo wakati huo walikuwa wameongezeka na kuwa sita kutoka watano waliokuwepo mwaka 1958. Mabadiliko hayo ni kama ifuatavyo:

5 EA Shilling


10 EA Shilling


20 EA Shilling



100 EA Shilling


Baada ya nchi zote za Afrika ya Mashariki kuwa huru, noti za kwanza zilizotolewa mwaka 1964 zilifanyiwa mabadiliko makubwa sana. Kwanza, noti hizi zilikuwa zimeandikwa katika Kiingereza, Kiarabu na Kishwahili; halafu sura ya Mtawala wa Uingereza iliondolewa na badala yake kuwekwa mashua. Sikuweza kufahamu mara moja kwa nini waliamua kutumia mashua. Sura za nyuma za noti ziliendelea kuonyesha mazao mbalimbali ya Afrika ya Mashariki ingawa kwa mpangilio tofauti kama ionekanavyo katika picha hizi.

5 EA Shilling


10 EA Shilling


20 EA Shilling


100 EA Shilling




Utawala wa Nyerere

Baada ya kuvunjwa kwa Bodi ya Sarafu ya Afrika ya Mashariki na kuundwa kwa Benki Kuu za Tanzania, Kenya na Uganda mwaka 1966, Benki Kuu ya Tanzania ilitoa noti za kwanza zenye thamani hizo hizo za Shilingi 5, 10, 20 and Shilingi 100. Upande wa mbele wa noti hizi kulikuwa na sura ya Mwalimu Nyerere wakati wa kupata Uhuru, na upende wa nyuma ulionyesha mambo mbalimbali yaihusuyo Tanzania. Noti ya Shilingi 5 ilikuwa na Mlima Kilimanjaro, noti ya Shilingi 10 ilikuwa na shamba la mkonge, wakati noti ya Shilingi 20 ilikuwa inaonyesha mgodi wa almasi wa Mwadui. Noti ya Shilingi 100 ilikuwa inaonyesha morani wa Kimasai akichunga ng'ombe wake (Hii ilifahamika sana kama Noti ya Mmasai).

5 Tz Shilling


10 Tz Shilling



20 Tz Shilling


100 Tz Shilling


Kwa waliotumia noti hizo wanakumbuka kuwa noti ya Shilingi 10 ilikuwa inajulikana pia kama 'Jani la Katani', wakati ile ya Shilingi 100 ilikuwa inajulikana pia kama 'Masai' au 'Pink' kutokana na rangi yake. Kwa muda mrefu noti ya Shilingi 20 imeendelea kujulikana kama pound au "mbao" kutokana na historia kuwa mwanzoni ilikuwa ina thamani ya Pound 1.
Hata hivyo sura ya Masai kwenye noti ilileta mjadala kidogo kiasi kuwa Benki Kuu iliamua kuzibadilisha. Ilipofika mwaka 1969, wakatoa noti za Shilingi 100 ambazo zilikuwa na wanyama katika Mbuga ya Serengeti kama ionekanavyo hapa chini:

100 Tz Shilling


Noti hizi ziliendelea kutumika hadi mwaka 1978 zilipofanyiwa mabadiliko makubwa hasa ili kuondoa sura ya kitoto ya Nyerere na kuweka picha ya Nyerere akiwa mtu mzima. Noti mpya zote zilikuwa zimendikwa kwa Kiswahili tu, na vile vile noti ya Shilingi tano ilisimamishwa. Upande wa nyuma wa noti zote kulikuwa na Ramani ya Tanzania pamoja na sura mbalimbali zihusuzo Tanzania. Noti ya Shilingi 10 ulikuwa na Mlima Kilimanjaro, kinyago cha kimakonde na mnara wa Azimio la Arusha; noti ya Shilingi 20 ilikuwa na kiwanda cha nguo kuashiria kuwa nchi ilikuwa inasonga mbele katika viwanda, na ile noti ya Shilingi 100 ilikuwa na tasisi za elimu kuanzia shule za msingi na vyuo vikuu kuashiria juhudi za nchi kupambana na adui ujinga. Vile vile shughuli za elimu ya kujitegemea zimeonyeshwa kwa wanafunzi kulima kwa jembe la mkono!

10 Tz Shilling


20 Tz Shilling


100 Tz Shilling


Miaka saba baadaye, mwaka 1985 (muda mfupi sana kabla Nyerere hajastaafu) noti zilifanyiwa mabadiliko tena kwa kuondoa noti ya Shilingi 10 na kuwekwa kwa noti ya Shilingi 50. Noti hizi zilikuwa na sura ya Nyerere akiwa ameanza kuzeeka, na zilitumia rangi nyingi sana kuliko zilizotangulia. Kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1958, noti ya Shilingi 100 ilibadilishwa rangi kutoka "pink" na kuwa ya bluu. Noti ya Shilingi 20 ilionyesha shughuli mbalimbali za baadhi ya viwanda vyetu, wakati Shilingi 50 ilionyesha shughuli za kujitolea kujenga mashule. Noti ya Shillingi 100 ilionyesha wasomi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya majengo ya chuo hicho. Nadhani ilikuwa pia kuonyesha kuwa nchi imepiga hatua katika upande wa elimu ya juu.

20 Tz Shilling


50 Tz Shilling


100 Tz Shilling


Utawala wa Mwinyi

Mwishoni mwa mwaka 1985 Nyerere alirudi kijijini kwake Butiama na kuiacha Ikulu mikononi mwa Mwinyi. Noti mpya zilizotolewa mwishoni mwa mwaka 1986 zilikuwa sawa kabisa na zile zilizoachwa na Nyerere isipokuwa zilikuwa na sura ya Mwinyi isipokuwa noti zile za Shilingi 100 ambazo ziliendelea kuwa na sura ya Nyerere kama Baba wa Taifa. Vile vile noti mpya ya Shilingi 200 ilianzishwa ikiwa inajulikana wakati huo kama "double cabin." Nyuma ya noti hizi za Shillingi 200 kulikuwa na wavuvi wanaodhaniwa kuwa walikuwa wa Zanzibar kwa vile kuna karafuu inayoonekana kwa pembeni.

20 Tz Shilling


50 Tz Shilling


100 Tz Shilling


200 Tz Shilling

Ilipofika mwaka 1988, kufuatia kushuka kwa thamani ya shilingi, ilikuwa ni muhimu kuwepo kwa noti zenye thamani kubwa zaidi ili kuwapunguzia watu mzigo wa pesa. Hivyo Benki Kuu ikaanzisha noti mpya za Shilingi 500, ambao zilijulikana kama "Pajero." Noti hizi za Shilingi 500 zilikuwa na sura tofauti kabisa na zile nyingine. Nembo ya Taifa ilikuwa ya rangi, halafu zilikuwa na nembo ya waziwazi ya Benki Kuu ya Tanzania. Nyuma yake zilionyesha akina mama wakivuna zao la kahawa au karafuu, sikumbuki tafsri ya picha hiyo vizuri.

500 Tz Shilling


Kasi ya kupungua kwa thamani ya shilingi ilikuwa kali sana kiasi kuwa miaka miwili baadaye, yaani mwaka 1990, Benki Kuu ililazimika kuingiza noti mpya ya Shilingi 1,000 ambayo ilikuwa na sura kama ile ya Shilingi 500 isipokuwa ngao ya taifa haikuwa ya rangi. Vile vile ilikuwa na maandishi ya ndani kwa ndani (water mark) kuonyesha 1,000. Nyuma yake kulikuwa kiwanda cha nyama cha Tanganyika Packers cha pale Kawe.

1000 Tz Shilling


Noti zetu wakati huo zilikuwa pana sana na zilikuwa zinaongezeka upana kadiri thamani yake inavyopanda. Ilipofika mwaka 1992, Benki Kuu ilifanya mabadiliko makubwa katika noti zetu. Kwanza zilipunguzwa sana upana halafu zote zikatengenezwa upya kuwa na sura inayofanana. Noti ya Shilingi 20 iliondolewa na badala yake zikaongezwa noti mbili za Shilingi 5,000 na Shilingi 10,000 kama ifuatavyo:

50 Tz Shilling


100 Tz Shilling


200 Tz Shilling


500 Tz Shilling


1000 Tz Shilling


5000 Tz Shilling


10000 Tz Shilling



Noti hizi ziliendelea kutumiwa hadi mwisho wa utawala wa Mwinyi mwaka 1995.


Utawala wa Mkapa na Kuendelea Hadi Leo

Wakati Mkapa alipochukua usukani wa kuongoza nchi mwaka 1995, aliamua kusitisha matumizi ya sura za viongozi kwenye noti (kwa kuwa yeye hakutaka iwekwe sura yake, kama alivyokataa kuitwa 'mtukufu rais' bali 'mheshimiwa rais'). Kwa hiyo noti zote zilizotolewa mwaka 1997 chini ya utawala wake hazikuwa na sura ya kiongozi yeyote. Badala yake zilikuwa na kichwa cha Twiga ambaye kihistoria ndiye Mnyama wa Taifa. Wakati huo pia, noti za Shilingi 50, 100 na Shilingi 200 zilisimamishwa.

500 Tz Shilling


1000 Tz Shilling


5000 Tz Shilling


10000 Tz Shilling


Hata hivyo, baada ya kifo cha Mwalimu Nyerere mwaka 1999, iliamuliwa kuwa sura yake iwe ya kudumu kwenye noti ya Shilingi 1,000, hivyo noti hiyo ilisanifiwa upya na kuwa kama ifuatavyo:

1000 Tz Shilling


Noti hizi ziliendelea kutumika hadi mwaka 2003 zilipofanyiwa mabadiliko ya kuongeza usalama zaidi. Vile vile kutokana na manung'uniko ya kichinichini kutokea Zanzibar kuhusiana na mtumizi ya Twiga ambaye alikuwa mnyama wa Tanganyika, iliamuliwa kutotumia twiga tena. Badala yake sura za wanyama wakubwa mbalimbali wa Tanzania zilitumika ingawa sura ya Nyerere iliendelea kubaki kwenye noti za Shilingi 1,000. Vile vile noti mpya ya Shilingi 2,000 ilianzishwa. Upande wa nyuma wa noti hizi ulionyesha shughuli mbalimbali za uchumi, sehemu za kihistoria na harakati za kukuza elimu. Kwa mara nyingine tena kuanzia mwaka 1978, noti hizi ziliandikwa kwa Kiingereza na Kishwahili tena. Noti hizi ndizo zinazotumika hadi leo, sura zake ni kama ifuatavyo:

500 Tz Shilling


1000 Tz Shilling


2000 Tz Shilling


5000 Tz Shilling


10000 Tz Shilling


Hatujui mabadiliko yajayo yatakuwaje hasa ikizingatiwa kwamba Shilingi yetu imeendelea kuporomoka thamani kila mwaka. Tusubiri na tuone.