Fatma Leonard 'akila kona'.
MSANII wa
filamu Bongo, Fatma Leonard wiki iliyopita alinaswa na paparazi wetu
akihamisha vitu vya ndani nyumbani kwa mpenzi wake huko Ubungo Makuburi
jijini Dar es Salaam akidai kuchoshwa na maisha bila ndoa. Hata hivyo,
paparazi lilikuta tayari mzigo wa fenicha umeshaondoka.
Msanii wa filamu Bongo, Fatma Leonard akifungasha virago kuianza safari.
“Nimemvumilia kwa muda mrefu sana, kila siku namkumbusha, sasa
inaonekana kama ninalazimisha, nimeamua kuchukua vyangu kwa sababu
nimempata mtu mwenye mapenzi ya kweli ambaye yupo tayari kunioa,”
alisema Fatma akikataa kulitaja jina la mpenzi wake huyo anayempotezea
muda.
Baba mwenye nyumba hiyo alimpigia simu mpangaji wake kumfahamisha kuhusu
kuondolewa kwa mizigo hiyo, lakini alimtaka amuache achukue anachotaka,
kitu kinachoonyesha aliridhia kitendo hicho kilichowavutia majirani
wengi waliojazana kushuhudia.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni