Jumla ya Mara Iliyotazamwa

20 Ago 2014

HATIMAYE MAHUSIANO YA WASTARA NA BOND YAPEWA BARAKA ZOTE NA AUNT LULU...!


BAADA ya kuachwa na mpenzi wake wa siku nyingi Bond, ambaye kwa sasa anadaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwigizaji wa filamu, Wastara Juma, Aunty Lulu amekubali yaishe na sasa hana tena kinyongo nao.
Mwigizaji wa filamu Bongo, 'Aunty Lulu'.
“Mimi sina tena kinyongo na Wastara, vile nilikuwa namfanyia tu vituko, lakini kwa sasa asiniogope wala asiwe na wasiwasi na mimi, nimeshaachana na Bond japokuwa tulitoka mbali sana na hakuna wanamke anayemjua kama mimi, siku ya harusi yao nitacheza mpaka asubuhi,”alisema Aunty Lulu.
Staa wa filamu Bongo, Wastara Juma akiwa na muigizaji mwenzake 'Bond'.
Msichana huyo aliyepata umaarufu baada ya kutwaa taji la Kimwana Twanga Pepeta, alitoa kauli hiyo hivi karibuni maeneo ya Kinondoni baada ya kutakiwa kutoa tamko juu ya uhusiano wa wawili hao, ambao awali alikuwa akiwatupia madongo na kuwapiga vijembe.
Alisema kwa sasa hana kinyongo na Wastara na amebariki uhusiano wao wa kimapenzi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni